KESI YA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA KIMBARI YAHAMISHIWA DAR ES SALAAM 

Mtuhumiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Innocent Sagahutu amepelekwa makao makuu ya uhamiaji mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Sagahutu alikamatwa hivi karibuni eneo la mpaka wilayani  Ngara alipokuwa akielekea Burundi.

Akizungumzia tukio hilo, Ofisa Uhamiaji mkoa wa Kagera Abdallah Tiwo alisema mtuhumiwa huyo amepelekwa makao makuu kwa ajili ya uchunguzi.  

“Ni kweli alikuwa anashikiliwa na uhamiaji mkoa wa Kagera,ila kwa sasa anaelekea Dar es salaam makao makuu ya uhamiaji.” alisema

Leave a comment